Saturday 13 March 2010

Breaking News

Meli ya Serengeti maarufu kama mkombozi wa Pemba imeteketea vibaya kwa moto jioni ya leo huko katika bandari ya Zanzibar, meli hiyo ilikuwa ikijitayarisha kupakia abiria kwenda Pemba, wakati tukio hilo likitokea kulikuwa na mabaharia 8 ambao saba walijiokoa kwa kuogolea wenyewe na mmoja akibaki ndani ya meli kwa kile kilichoelezwa kuwa hakuwa akijua kuogolea, hadi hivi sasa chanzo cha moto huo hakijaweza kufahamika, kwa mujibu wa mashuhuda wa moto huo wamesema moto ulianza katika chumba cha engine, juhudi ya fire kuuzima moto huo zilishindikana kutokana na kutokuwa na vifaa vya kuzima moto ndani ya bahari, mwaka jana pekee kulitokea ajali tatu za meli za mizigo na abiria kuwaka moto ambazo ni aziza one na two pamoja na meli ya MV Pemba

No comments: