Monday 22 February 2010

Asilimia 54 Wajiandikisha Kupiga Kura Zbar Awamu ya Kwanza

Jumla ya wapiga kura wapya laki mbili na elfu 71, 376 wamejiandikisha katika daftari la wapiga kura Zanzibar kwa awamu ya kwanza iliyoanza mwaka jana hadi Februari 14 mwaka huu.
Kwa mujibu wa takwimu za tume ya uchaguzi Zanzibar undikishaji huo umepata mafanikio kwa asilimia 53.50 ikilinganishwa na unadikishaji wa wapiga kura uliofanyika mwaka 2005 ambapo tume hiyo ilisajili wapiga kura wapya laki mbili, elfu 35, 849.Kazi za uandikishaji ambazo kwa sasa zimo katika matayarisho kwa awamu ya pili, tume ya uchaguzi imekadiria kuandikisha zaidi ya asilimia 46.50 ya wapiga kura kwa Unguja na Pemba.Katika uandikishaji huo wa awamu ya kwanza ya wapiga kura wapya Kisiwa cha Unguja kimeonesha kuwa na idadi kubwa ya wapiga kura waliofikia laki mbili, elfu tisa na 49 wakati Pemba watu waliojiandikisha ni elfu 63, mia tatu na 27.

Habari kwa hisani ya Zenj Fm Zanzibar

No comments: