Monday 22 February 2010

Wastaafu Watakiwa Kuwapisha Vijana Zanzibar

Serikali ya mapinduzi Zanzibar imeshauriwa kuachana na mpango wa kuwaongezea muda watumishi wake wanaostaafu hatua ambayo itawasaidia vijana kupata nafasi za ajira. Mwenyekiti wa chama cha siasa cha AFP Said Soud Said amesema vijana wengi wanaomaliza masomo yao wanakosa nafasi za ajira serikalini kwa kisingizio cha kukosa uzowefu. Amesema endapo serikali itaendelea na mpango huo, taifa litabeba mzigo mkubwa kutokana na baadhi ya vijana kujihusisha na vitendo viovu wakati wanapokosa ajira. Hata hivyo amesema baadhi ya wafanyakazi wanastahiki kuongezewa muda kama vile madaktari, lakini sio kwa taasisi nyingine. ……CLISP…(SAVED-SAID

kwa hisani ya Zenj Fm

No comments: