Monday 22 February 2010

DNA Bado Kitendawili Zanzibar

Wizara ya afya na ustawi wa jamii Zanzibar imesema imeshatafuta Mtaalamu maalum watakao fanya utafiti juu ya kuwepo kipimo cha DNA nchini ili kuondosha usumbufu mkubwa katika upatikanaji wa kipimo hicho. Katibu mkuu wizara ya Afya na ustawi wa Jamii Zanzibar Mohammed Saleh Jidawi amesema hayo katika mkutano wa uzinduzi wa kitengocha hifadhi ya mtoto iliyozinduliwa katika hoeli ya zanzibar ocen view kilimani mjini zanzibar. ….CLIP(SAVED-JIDAWI). Aidha ametoa wito kuwepo kwa ushirikiano na taasisi mbali mbali nchini pamoja washirika wa maendeleo kushirikiana katika utoaji wa elimu kwa wanachi juu ya haki za watoto.
Nae katibu mkuu wizara ya elimu na mafunzo ya amali Mwanaidi Saleh ameitaka jamii kubadilika na kuelekeza nguvu zao katika kutokomeza tatizo la ubakaji …..CLIP(SAVED-WEMA)
Aidha amekitaka kitengo hicho cha uhifadhi wa watoto kuandaa muongozo maalum wa kitaifa ili kuendeleza ustawi wa watoto.\ Na Zenj fm

No comments: